• This is default featured slide 1 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 2 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 3 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 4 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 5 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Friday, August 12, 2016

Panda Mpunga kwa nafasi ili upate mavuno zaidi na uokoe gharama ya mbegu


Panda kwa nafasi zilizopendekezwa na wataalamu. Kumbuka kuwa na idadi ya mimea inayopendekezwa shambani ni chanzo cha mavuno mengi kwani wingi wa mimea unamaanisha wingi wa wazazi shambani.
Panda kwa msitari ili kurahisisha zoezi la palizi, utiaji mbolea na uvunaji.
Nafasi zitumikazo kupanda mpunga shambani.
Nafasi kati ya shina na shina (Sm)
Idadi ya mimea katika Ekari
Idadi ya mimea katika Hekta
20 kwa 20
100,000
 250,000
15 kwa 15
177,778
 444,444
15 kwa 20
133,333
 333,333
25 kwa 25
 64,000
 160,000
25 kwa 20
 80,000
 200,000
Hata hivyo, uchaguzi wa vipimo vya kutumia shambani hutegemea:
a.    Aina ya mbegu, ndefu-mbali mbali, fupi – karibu karibu

b.    Rutuba ya shamba, rutuba nyingi – karibu karibu, rutuba kidogo – mbali mbali
Share:

FAHAMU KILIMO BORA CHA ALIZETI

Image result for alizeti

Utangulizi

Alizeti ni zao mojawapo kati ya mazao muhimu yanayotoa mbegu za mafuta. Hutoa mafuta kati ya asilimia 40 – 45 na mashudu yake ni chakula cha mifugo. Alizeti huvumilia ukame na hulimwa kwa ajili ya biashara na matumizi ya nyumbani. Wakulima huvuna kiasi kidogo, kati ya gunia 3 – 5 kwa hekta. Hivyo kwa mavuno mengi na bora, mkulima anashauriwa kuzingatia mambo yafuatayo:-

Kuandaa Shamba

Unashauriwa kutayarisha shamba lako mapema kwa kukatua ardhi na kulainisha vizuri. Samadi yaweza kuchanganywa vizuri na udongo wakati wa kuandaa shamba.
www.ariuyole.go.tz

Wakati wa Kupanda

Upandaji wa alizeti hutegemea sana hali ya hewa ya eneo husika.
Maeneo yenye mvua nyingi alizeti huanza kupandwa mwishoni mwa mwezi Januari mpaka katikati ya
mwezi Februari.
Maeneo yenye mvua kidogo alizeti hupandwa mwezi Desemba hadi Januari.

Kiasi cha mbegu na upandaji

Kiasi cha kilo 3 – 4 za mbegu zinatosha kupanda eneo la ekari moja.
Panda mbegu 3 – 4 katika kila shimo moja kwa nafasi ya sentimita 75 kutoka mstari hadi mstari na sentimita 30 kutoka shimo hadi shimo. Shimo la mbegu liwe na kina cha sentimita 2.5 – 5.
Wiki mbili baada ya kuota, punguza miche katika kila shimo na kubakiza mche mmoja.

Kiasi cha mbolea

Mbolea zinazofaa kwa kilimo cha alizeti ni zile za kupandia na kukuzia hasa kwenye maeneo yasiyo na rutuba.
Wakati wa kupanda tumia nusu mfuko kwa ekari moja ya mbolea ya kupandia na mfuko mmoja kwa ekari moja ya mbolea ya kukuzia kwa kuigawa mbolea hiyo mara mbili. Nusu ya kwanza iwekwe wakati wa kupanda na nusu ya pili iwekwe wiki mbili baadaye.
Wakati wa kuweka mbolea angalia isigusane na mbegu au mche wa alizeti kwani huunguza.

Palizi

Alizeti hukua taratibu katika wiki chache za mwanzo. Hivyo unashauriwa kupalilia mapema ili kupunguza
hasara. Katika maeneo yaliyo na magugu machache, palizi moja tu inatosha. Vile vile maeneo yenye upepo
mkali, wakati wa kupalilia inulia matuta ili kuzuia kuanguka.

Wanyama na wadudu Ndege

Alizeti hushambuliwa sana na ndege ambao huweza kuteketeza hadi asilimia 50 ya mazao shambani.

Kuzuia

- Usipande alizeti karibu na msitu/pori
- Vuna mapema mazao yako mara tu kichwa kinapobadilika rangi na kuwa manjano
- Panda alizeti kwa wingi katika shamba moja
- Amia ndege kwa mutumia sanamu, makopo na ua kuweka watu ingawa ni gharama.

Funza wa vitumba (American bollworm)

Funza huyu hutoboa mbegu changa kuanzia mara tu vitumba vya maua vikifunguka mpaka karibu na
kukomaa kwa mbegu.

Kuzuia:

- Tumia dawa yo yote ya kuulia wadudu inayopatikana katika eneo lako.
Magonjwa
Alizeti hushambuliwa na magonjwa yakiwemo madoa ya majani, kutu, kuoza kwa mizizi, shina, 
 

kichwa na kushambuliwa na virusi.


www.ariuyole.go.tz

Kuzuia:

- Tumia kilimo cha mzunguko wa mazao
- Panda mbegu safi zilizothibitishwa na wataalamu
- Choma masalia ya msimu uliopita

Uvunaji

Unashauriwa kuvuna alizeti mara tu inapokomaa ili kupunguza hasara ya kushambuliwa na ndege. Alizeti iliyokomaa kichwa hubadilika rangi toka kijani kibichi na kuwa njano. Kata vichwa na kuvianika juani ili vikauke vizuri.
Piga piga vichwa ili kutoa mbegu za alizeti, kisha upepete na kuendelea kuzianika ili zikauke vizuri.
Utafiti unaonyesha kuwa mkulima anaweza kupata magunia kati ya 10 -12 kutoka katika ekari moja.

Kwa Mawasiliano zaidi wasiliana na:

Taasisi ya Utafiti Uyole,
Kitengo cha mbegu za Mafuta
S.L.P. 400
MBEYA
Simu: 025 2510062
Fax: 025 2510065
Barua pepe; ariuyole@iwayafrica.com
website: www.ariuyole.go.tz
www.ariuyole.go.tz
Share:

MADHARA YA KUTUMIA KEMIKALI NYINGI SHAMBANI







Wakulima wamekuwa wakitumia kemikali kiasi cha kutisha kwenye mazao kwa ajili ya kudhibiti wadudu.
Kwa mfano uzalishaji wa nyanya unaweza kuwa na faida kwa mkulima. Msimu ambao nyanya zinakuwa chache bei hupanda mkulima anapata faida zaidi. Kwa upande mwingine zao la nyanya ni rahisi sana kushambuliwa na wadudu na magonjwa.
Tatizo moja kubwa la kutumia dawa za kudhibiti wadudu na magonjwa  kwa kiasi kikubwa ni kuwa wadudu hao huwa sugu baada ya muda mfupi. Wakulima kwa uoga wamebuni njia yao wenyewe ya kudhibiti wadudu na magonjwa. Imetushangaza na kutushtua kugundua kuwa baadhi ya wakulima hapa nchini wanatumia dawa ya kuulia kupe kwa ajili ya kuua wadudu wa nyanya kama vile inzi weupe, vithiripi, utitiri na buibui.
Dawa hii inaruhusiwa kutumika kwa ajili ya kuogeshea wanyama tu lakini si kwenye mboga ambazo zinauzwa kwa walaji.
Sokoni kuna aina nyingine za dawa ambazo ni hatari na zilishapigwa marufuku na serikali, lakini cha kushangaza baadhi ya maduka ya pembejeo bado yanaziuza na wakulima wanatumia.
Aina hizi za kemikali ni hatari sana kwa afya ya binadamu hasa zinapojikusanya kwa kiasi kikubwa mwilini. Baada ya muda mrefu inaweza kuwa sugu na kusababisha magonjwa ambayo pia ni sugu ambayo hata sasa yamekuwa tatizo kubwa katika baadhi ya maeneo hapa nchini, kwa mfano saratani, ukuaji usiokuwa wa kawaida kisukari na magonjwa ya mzio.
Mbali na madhara kwa afya ya binadamu, pia sumu hizo hupenya na kwenda kwenye maji yaliyomo ardhini na kuyachafua. Sumu hizo huathiri na kuuwa wadudu muhimu waliomo ardhini ambao huboresha udongo, kuuwa wadudu muhimu ambao hufanya ushavushaji kwenye mazao, na wadudu wengineo ambao hudhibiti wadudu waharibifu kwenye mazao na mazingira yetu.
Njia endelevu za kudhibiti wadudu
Kuna mbinu za kudhibiti wadudu ambazo ni salama kwa mazingira yetu. Njia hizo zinajumuisha matumizi ya wadudu rafiki kama vile nyigu, bungo na wengineo kwa ajili ya kudhibiti wadudu hawa.
Endapo wakulima wataacha kutumia kemikali hizi, wadudu hawa wataweza kudhibiti wadudu hao waharibifu kwa asili. Endapo madhara makubwa mkulima anaweza kutumia dawa za asili katika kudhibiti wadudu hawa, dawa ambazo hazina madhara yoyote.
Tumia dawa za asili
Mojawapo ya wadudu ambao huwa wakulima hupata shida kuwadhibiti, ni inzi weupe, vithiripi, buibui wekundu, na vidukari. Wadudu hawa huharibu kati ya asilimia 20-30 ya mazao na kuendelea. Wadudu kama vithiripi na inzi weupe ni vigumu sana kuwadhibiti kwa kuwa huzaliana kwenye mazao yanayokua. Hivyo tumia njia ya  kujihami kabla.
Badala ya wakulima   kutumia kemikali, wanaweza kutumia dawa za asili ambazo haziui wadudu rafiki na ambazo pia husaidia mimea kujijengea kinga dhidi ya magonjwa.
Kuandaa dawa za asili:
Mkulima  anaweza kutumia aina nyingi za  mimea katika kutayarisha dawa za asili.  Mfano wa mimea hiyo ni pamoja na bangi mwitu, tangawizi, mlonge, Mwarobaini na pareto. Katakata mimea  yote hiyo kwenye debe na uloweke kwenye pipa lenye ujazo wa lita 200.
Jaza maji kwenye pipa hilo na uchanganye kwa nguvu sana. Funika pipa hilo vizuri uhakikishe hakuna hewa inayopita. Ongeza lita moja ya EM na lita 4 za molasesi. Vundika kwa muda wa siku 7-10. Weka mchanganyiko wa mimea ya dawa kwenye bomba la lita 20 lililojazwa maji. Nyunyiza kwenye mazao yako angalau mara tatu kwa wiki. Dawa za asili zinaweza kukinga mazao yako dhidi ya wadudu wote na hata magonjwa, pamoja na kupata mazao ambayo ni salama kwa afya.
Share:

WADUDU WAHARIBIFU NA MAGONJWA MBALI MBALI KATIKA ZAO LA KABICHI


 




WADUDU WAHARIBIFU
 Viwavi wa kabichi: Hawa ni viwavi wenye rangi ya kijani na alama ya mstari wa kung’aa mgongoni. Nondo hutaga mayai chini ya jani na baada ya kuanguliwa viwavi hawa hula sehemu ya chini ya jani na kucha ngozi nyembamba mfano wa dirisha la kioo. Ni muhimu kuwadhibiti viwavi hawa kwa sababu ndio wanaoleta madhara makubwa. Viwavi wa kabichi huzuiwa kwa kunyunyizia moja ya dawa zifuatazo:- Nogos, Permethrin,Dimethoate, Sevin W.P. na Sumicidin.
 
Nzi wa Kabichi: Mashambulizi hufanywa na kiluwiluwi mwenye rangi ya kijani au bluu. Hula majani yote ya kabichi na kubakisha vena au vishipa vya majani. Inzi wa kabichi wanaweza kuzuiwa kwa kutumia dawa za Sevin, Dimethoate, Permethrin na Fenvalerate(sumicidin)
 Sota: Hawa ni funza wakubwa wenye rangi ya kijivu. Hupendelea kujichimbia katika udongo wakati wa mchana na kukata miche michanga karibu na usawa wa ardhi wakati wa usiku. Zuia wadudu hawa kwa kutumia majivu au dawa kama vile Carbaryl, Fenvalerate au Decis mara baada ya kuotesha. Kama mche utakatwa, mtoe mdudu huyu kwa kumfukua na kumuua. Kisha pandikiza mche mwingine. 
Vidukari au wadudu mafuta:  Wadudu hawa ni wadogo sana wenye rangi ya kijani, nyeusi au khaki.  Baadhi yao wana mabawa na wengine hawana. - Hufyonza utomvu wa mimea na husababisha majani kubadilika rangi na kuwa meupe au njano iliyopauka.  Mmea hudumaa na hatimaye hukauka. Zuia kwa kunyunyiza mojawapo ya dawa hizi Fenvalerate, Dimethoate, Karate, Nogos
Minyoo Fundo: Ni minyoo wadogo wanaoishi ardhini na ambao hawaonekani kirahisi kwa macho. Hushambulia mizizi na kusababisha kabichi kudhoofu na kushindwa kufunga vizuri. Mimea iliyoshambuliwa, mizizi yake huwa na nundunundu. Kuzuia: Matumizi ya mbolea za asili kila msimu husaidia kupunguza kuzaliana kwa wadudu hao. - Tumia mzunguko wa mazao, usiotesha zao la jamii ya kabichi baada ya kuvuna kama vile kabichi ya kichina, koliflawa,n.k Otesha mboga kama vile karoti, radishi, vitunguu au mahindi. - Ondoa masalia yote shambani ambayo yanaweza kueneza wadudu hawa na yachome moto.
 MAGONJWA
 Kuoza shingo; Husababishwa na vidudu vya bacteria ambavyo viko kwenye udongo. Hushambulia kabichi na kuzifanya zibadilike rangi.  Kuoza na kutoa harufu mbaya. Vidudu vidovidogo huonekana pia kwenye sehemu iliyooza. Kuzuia:
·        Epuka kujeruhi kabichi wakati wa kuvuna.
·        Vuna kabichi wakati hakuna mvua - Usilundike kwa wingi na kwa muda mrefu.
·         Hifadhi kwenye sehemu yenye ubaridi na hewa ya kutosha.
·        Ng’oa masalia, choma moto na lima shamba mara moja baada ya kuvuna - Tumia mzunguko wa mazao. 
 Uozo Mweusi;  husababishwa na Bakteria . Majani hugeuka kuwa njano na baadaye kuwa kahawia . Majani huanza kunyauka kutoka kwenye kingo zake na kuacha alama ya “V” yenye rangi nyeusi isiyokolea.  Baadaye majani hunyauka na kupukutika. Kama ukikata jani au shina, mviringo mweusi huonekana kwenye vena.
Kuzuia:
·        Badilisha mazao.
·        Usipande kabichi au jamii yake kwa muda wa miaka 2 kwenye eneo lililoadhirika.
·        Otesha kabichi kwenye sehemu ambayo haituamishi maji.
·         Kitalu na mazingira yake viwe safi daima.
·        Punguza miche ili kupunguza msongamano.
·         Ondoa masalia yote baada ya kuvuna ya yachomwe moto.
·        Otesha mbegu zilizodhibitishwa na wataalam.
 Kuoza shina; Ni ugonjwa waukungu, Madoadoa yaliyodidimia yenye rangi ya kahawia huonekana kwenye shina karibu na usawa wa ardhi, ikifuatiwa na kuvimba kwa shina.  Baadaye uyoga mweusi huonekana kwenye uvimbe huo. Uozo wa rangi ya kahawia huonekana ndani ya shina.  Majani huwa na madoa meusi ya mviringo yaliyozungukwa na uyoga mweusi.
 Kuzuia:
·        Otesha kabichi sehemu ambayo haituamishi maji.
·         Badilisha mazao, usioteshe kabichi kwenye eneo lililoathirika kwa muda wa miaka 3.
·         Lima shamba mara baada ya kuvuna ili kuwezesha masalia kuoza haraka kabla ya kuotesha tena.
·         Ondoa kabichi zote zilizoshambuliwa shambani.
·        Tumia dawa ya kuzuia ukungu kama vile Ridomil. 
 Uvimbe wa mizizi; Husababishwa na ukungu. Hushambulia mizizi na dalili zake ni kudumaa kwa mmea na majani kukunjamana . Baadae mmea huoza
Kuzuia: Badilisha mazao shambani.
Madoa Meusi:  Chanzo ni ukungu. Majani huwa na madoa madogo madogo ya mviringo yenye rangi ya njano .  Baadae madoa huwa makubwa na hugeuka kuwa meusi.
Kuzuia:
·        Badilisha mazao
·         Hakikisha shamba ni safi wakati wote
·         Ikibidi tumia dawa za ukungu kama vile Kocide,Cupro, n.k. ·
·        Ubwiri
 Vinyoya:  Ni ugonjwa wa ukungu. Hupendelea hali ya unyevunyevu na baridi kali. Huanzia kwenye kitalu . Mabaka ya mviringo yenye rangi ya njano huonekana upande wa juu wa jani. Baadae hubadilika na kuwa rangi ya zambarau iliyochanganyika na nyeupe upande wa chini wa majani.
Kuzuia:
·        Tumia mzunguko wa mazao.
·        Hakikisha udongo hautuamishi maji na kitalu ni kisafi wakati wote.
·         Tumia za ukungu kama Zineb, Didhane, M45, Kocide, Topsin-M na Ridomil.
Kuoza shina au Kinyaushi: Husababishwa na ukungu. Hushambulia miche michanga. Miche iliyoshambuliwa huonyesha dalili za kukauka. Miche mikubwa huonyesha dalili za kudumaa. Sehemu ya shina iliyo karibu na ardhi hulainika na kuwa rangi ya kahawia.
Kuzuia:
Punguza miche kama imesongamana. Nyunyiza dawa ya ukungu Kama Didhane M-45, Ridomil, Topsin-M.
Share:

FAHAMU KILIMO BORA CHA MATANGO


Kilimo cha Tango

ni zao linalopendelea hali ya hewa ya joto na husitawi vema kati ya nyuzi joto 18°C hadi 35°C
Udongo Hustawi vizuri katika udongo tifutifu wenye rutuba usiotuamisha maji
Maandalizi ya shamba Lima shamba kwa trekta, kwa ng’ombe ama kwa jembe la mkono kwa kina cha sentimita 30 hadi 45
Weka matuta ya mwinuko yenye upana wa mita 1 hadi 1.5 kutoka kati ya tuta na tuta
Upandaji Zipo aina mbili za upandaji,
1.ya kwanza ni ile ya kupanda mbegu moja kwa moja na
2. ya pili ni ile ya kupanda mbegu katika trei na kuhamisha baada ya siku 8 hadi 10.
 
Njia ya kupanda mbegu moja kwa moja ni rahisi lakini ile ya kupanda katika trei ni bora zaidi kwani shamba hujaa vizuri katika nafasi na hukua haraka na kuzaa mavuno mengi
Pima mashimo ya kupandia katika umbali wa sentimita 20 hadi 25 kutoka shina hadi shina mstari mmoja kwa tuta na sentimita 40 katika mfumo wa zig-zag pande zote mbili za tuta na kupanda
Mbolea kianzio iwekwe katika kila shimo na kupanda endapo miche kutoka katika trei itatumika Hakikisha shamba lina unyevu wa kutosha kabla ya kupanda
Palizi Palilia shamba mara kwa mara ili kuhakikisha shamba halina magugu Magugu hudhibitiwa kwa palizi ya jembe, kung’oa kwa mkono ama matumizi ya viuagugu.
Njia nyingine ni matumizi ya plastiki maalum kuzuia magugu yaani ‘plastic mulch’
Mbolea Tumia mbolea ya DAP wakati wa kupanda na kisha tumia NPK yenye uwiano mmoja kama, 18:18:18, 17:17:17 ama 16:16:16 baada ya wiki tatu toka Usegekaji
Tumia nguzo za unene wa inchi 2 na kamba ili kuinua mimea na matunda yasiguse ardhi na kuoza

Uchavushaji

Hii ni muhimu sana kuzingatiwa kwani tango huchavushwa kwa wadudu na si upepo
.Bila wadudu kama nyuki uzalishaji huathrika sana.
Ni muhimu kupanda mazao kama alizeti na maua mbali mbali yanayopendwa na wadudu wachavushaji ili kuhakikisha uwepo wa wadudu hao shambani.
Aidha inapo-lazimu ni vema kuweka mizinga kadhaa ya nyuki katika shamba la tango
Matumizi ya viuatilifu Katika udhibiti wa wadudu na magonjwa matumizi ya viuatilifu yafanyike kwa maelekezo ya wataalam
kubaini tatizo na kiuatilifu hitajika na namna ya matumizi yake
Mavuno Mavuno huanza baada ya siku 40 hadi 45 kutegemea na aina pamoja na hali ya hewa...
Share:

FAHAMU KILIMO BORA CHA KABICHI



 Zao la kabichi hulimwa katika mikoa ya Morogoro, Arusha,Tanga, Iringa, Kilimanjaro na Mbeya. Kama mboga zao la kabichi lina viini lishe kama chokaa, protini, kambakamba na maji kwa wingi. Hutumika kutengeneza kachumbari, pia kuchanganywa na nyama au maharage.
HALI YA HEWA
Zao la kabichi hupendelea: hali ya ubaridi Mwinuko: Kuanzia mita 1200 hadi 1900 kutoka usawa wa bahari. Udongo uwe; Tifutifu,  Rutuba nyingi na Unaohifadhi unyevu kwa muda mrefu, Usiotuamisha maji , Usio na chumvichumvi nyingi. Kama hauna rutuba ya kutosha ongeza mbolea ya samadi au mbolea vunde. 
 AINA ZA KABICHI
 Early Jersey Wakefield:  Umbo lilochongoka kidogo, Hufunga vizuri,  Uzito ni kati ya kilo 1.5 hadi 2.0,  Hukomaa mapema siku 90 – 100 tangu kupandikiza. · Copenhagen Market: Vichwa vya mviringo na hupasuka kirahisi . Hukomaa mapema, siku 90 – 100 tangu kupandikiza ·
 Prize Drumhead: Vichwa vikubwa (kilo 2- 2.5), Vichwa ni bapa, huchelewa kukomaa (siku 110 – 120) - Huvumulia hali ya jua kali, Pia vichwa hupasuka. · Oxheart: - Vichwa vidogo huchongoka kama moyo,  Hupendwa sana na walaji,  Ladha yake ni tamu, hukomaa mapema, Hazina tabia ya kupasuka.  Glory of Enkhuizen: - Vichwa vya mviringo, Huvumilia hali ya jua kali,  Huchelewa kukomaa (siku 110 – 120)  na  Ina tabia ya kupasuka.
KUOTESHA MBEGU
Mbegu za kabichi huoteshwa kitaluni na baadaye huhamishiwa shambani. Andaa kitalu vizuri na weka mbolea za asili zilizooza vizuri kwa kiasi cha ndoo 5 – 10 za ujazo wa kilo 20 kwenye eneo la mita za mraba 10. Changanya na udongo kisha lainisha udongo kwa kuvunja mabonge makubwa kwa kutumia reki. Tengeneza tuta lililoinuka kwa sentimita 25 na lenye upana wa mita 1.
Mwagilia maji kwenye tuta siku moja kabla ya kusia mbegu. Kiasi cha mbegu zinazohitajika ni gramu 1 kwenye eneo la mita 1 ya mraba hivyo hekta 1 huhitaji gramu 200 – 300. Sia katika umbali wa sentimita 15 toka mstari hadi mstari na kina cha nusu sentimita.Funika mbegu na udongo laini kasha tandaza nyasi kazu ili kuhifadhi unyevu.Mwagilia maji kila siku asubuhi na jioni mpaka mbegu ziote, huota kwa muda wa siku 5 – 10.
KUTAYARISHA SHAMBA
Shamba litayarishwe mwezi mmoja kabla ya kupandikiza.
·        Katua ardhi kwa kina cha sentimita 30
·        Lainisha udongo na tengeneza matuta  kisha weka mbolea za asili kwa kiasi cha ndoo 2 kwa kila hatua moja au Mbolea iwekwe kwa kila shimo kwa kiasi cha kilo kwa shimo.
·         Mbolea ya N.P.K. 5:15:5 yaweza kuwekwa kwa kiasi cha kijiko 1 cha chai chenye gramu 5 kwa kila shimo.
KUPANDIKIZA MICHE
 
 
 Miche huwa tayari kupandikizwa shambani baada ya wiki 3 – 5 tangu kusia mbegu . Miche huwa na urefu wa sentimita 15 – 20. Ng’oa miche kwa uangalifu na pandikiza kama ilivyokuwa kitaluni na hakikisha mizizi haipindi wakati wa kupandikiza. Nafasi ya kupandikiza: Hutegemea aina ya kabichi – zenye vichwa vikubwa (Drumhead) ni sentimita 60 kutoka mche hadi mche na sentimita 75 toka mstari hadi mstari. – Zenye vichwa vidogo (Oxheart) ni sentimita 40 – 50 kutoka mche hadi mche na sentimita 60 toka mstari hadi mstari. – Umbali toka tuta moja na jingine ni sentimita 60. – Muda mzuri wa kuotesha ni asubuhi au jioni – Baada ya kupandikiza weka matandazo kama vile nyasi kavu ili kuhifadhi unyevu na kuzuia magugu kuota kwa urahisi. 
 PALIZI
 Zao la kabichi halina mizizi ya kina kirefu hivyo wakati wa palizi ni muhimu kuwa mwangalifu kwa kupalilia juu juu ili kuepuka kukata mizizi. Kuongeza matandazo husaidia kupunguza palizi a mara kwa mara.
UMWAGILIAJI
 Kabichi hustawi vizuri zaidi iwapo kuna maji ya kutosha kwenye udongo. Mwagilia mara mbili au zaidi kwa wiki kutegemea hali ya hewa na aina ya udongo. Kabichi ambazo hazikupata maji ya kutosha huchelewa kufunga na huwa na vichwa vidogo. Zikikosa maji kwa muda mrefu na zikapata maji mengi ghafla, vichwa hupasuka. 
 MBOLEA
Mbolea ya kukuzia (S/A) huwekwa baada ya 4 – 6 baada ya kupandikiza miche na kabla ya vichwa havijaanza kufunga. Kiasi cha kilo 80 huhitajika kwa eka moja. - Kilo 40 ziwekwe baada ya wiki 4 – 6 na kilo 40 ziwekwe tena baada ya mwezi mmoja . Mche mmoja huhitaji kiasi cha kidogo cha gramu 5. Mbolea iwekwe kuzunguka shina umbali wa sentmita 10 – 15 kutoka kwenye shina. Muhimu: Epuka kuweka mbolea nyingi, kwani husababisha vichwa visifunge vizuri (kabichi zinakuwa nyepesi) 
 KUBADILISHA MAZAO
 Kabichi nizao linalotumia virutubisho vingi kulinganisha na mboga nyingine,hivyo kabla ya kuotesha kabichi panda mazao jamii ya mikunde ili kuongeza rutuba. Baada ya kuvuna kabichi otesha mazao yanayotumia chakula kidogo kama vile karoti, radishi au lettuce. Kubadilisha mazao pia hupunguza kuenea kwa wadudu waharibifu na magonjwa. 
KUVUNA
 
 Kabichi hukomaa katika siku 60 mpaka 210 tangu kupandikiza miche. Hata hivyo muda wa kukomaa hutegemea aina ya kabichi. Uvunaji hufanyika kwa kukata shina sentimita 2 – 3 kutoka kwenye kichwa kwa kutumia kisu. Ondoa majani ya nje na acha majani 2 au 3 ya kijani kwa ajili ya kuzuia kabichi zisikwaruzike na kuoza wakati wa kusafirisha. Punguza urefu wa majani ili kurahisisha ufungaji. Ni muhimu uvunaji ufanyike asubuhi au jioni. Ondoa kabichi zilizooza au kuharibika wakati wa kuvuna, kisha panga zilizobaki kufuata daraja kama vile ndogo, za kati na kubwa. Mavuno: Kiasi cha tani 40 au zaidi za kabichi hupatikana kwa hekta moja kama zao limetunzwa vizuri.
HIFADHI
Kabichi ni zao linaloharibika kwa haraka, hivyo halina budi kutumika mapema iwezekanavyo baada ya kuvuna. Kabichi kwa ajili ya kuuzwa zisafirishwe mara moja kwa walaji. Kama usafiri ni mgumu, zihifadhiwe kwenye sehemu yenye ubaridi na hewa ya kutosha. Wakati wa kusafirisha, ziwekwe kwenye matenga au visanduku vya mbao vilivyo na matundu yanayoingiza hewa ya kutosha. leo tuishie hapa unaweza kuandika chochote au kutoa ushauri
Share:

FAHAMU KILIMO BORA CHA MATIKITI MAJI


Tikiti maji ni mboga/tunda linalolimwa hasa katika maeneo ya joto lenye kiwango cha joto cha 22-28 0c na mvua 600 - 400mm kwa mwaka. 
Matikiti yanahitaji hali ya hewa yenye joto na mwangaza wa jua wa kutosha . Kiwango kidogo cha unyevu kwa sababu unyevu mwingi unasababisha maradhi.  Unyevunyevu    mwingi unaadhiri ubora na utamu wa tunda. Vilevile, yanastawi vizuri katika aina mbalimbali za udongo wenye rotuba ya    kutosha na wenye kupitisha maji vizuri.

Aina  za matikiti maji


 NEGRA F1

Aina hii ya matikiti maji ni ya  mviringo yenye mazao na sifa nzuri”
Ubora wake
 • Yana mazao mazuri, na uwezo wa kukupa tani 46 kwa kila ekari
• Ni matamu sana na yenye wekundu wa kung’ara
 • yanakomaa katika muda wa siku 100-120
• Ni mviringo na yenye rangi ya kijani kibichi na hutoa matunda yenye  mizani kati ya kilo 7-10
 • Mmea hukua haraka na una mazao mazuri
 •Yamezungukwa na nyama ngumu, nzuri, yenye kukuwezesha  kusafirisha hadi sehemu za mbali
 • Yana kinga dhidi ya  ugonjwa wa mnyauko unaosababishwa na  vimelea aina ya Fusari (Fusarium wilt)

SENTINEL F1 


  ni aina mpya ya matikiti ya mviringo marefu” 
Ubora wake

• yanaweza kuzaa sana hadi tani 50 kwa kila ekari
• Ni marefu, yameshiba na yana rangi ya pundamilia
 • ni tamu, yan wekundu uliokolea na nyama iliyo na maji mengi
 • Yanawezakutoa matunda ya kufanana na yaliyo na uzani kati kilo 11 - 14
• Matunda yana nyama nyingi na umbo inayokuwezesha kusafirisha masafa marefu
 • yana kinga dhidi ya maradhi ya vimelea aina ya Fusari (Fusarium wilt Race 1)
 • yanakua tayari katika muda wa siku 100 -120 
Mbali na kuwa na faida mbali mbali kiafya tikiti maji linaweza kumtoa mkulima wa kawaida katika umaskini. Hii kutokana na sababu zifuatazo.
·   Tikitimaji ni zao la bustani linalochukua miezi 3-4 kuvunwa, hivyo kwa mwaka linaweza kuvunwa mara 3 hadi 4
·         kwa ekari moja mavuno ya tikiti maji ni matunda 2000 - 8000  au zaidi kwa miezi 3-4 kutokanana uangalizi wa mkulima katika shamba ikiwa ni kutumia mbolea kama inavyo takiwa, kuzuia wadudu na magonjwa, n.k. Pamoja na nafasi iliyotumika katika upandaji (1x1m, 2x2m, 1.5 x 1.5m).

JINSI YA KUJUA FAIDA

Katika maeneo mengi ya Tanzania bei ya tikiti maji lenye sifa nzuri ni shilingi 2,000/= hadi 3,000/=
kwa bei ya 2,000/= na mavuno ya 2000 matunda/ekari (Matunda mazuri)
Baada ya mavuno utajipatia kiwango cha chini kisichopungua jumla ya Tsh.4,000,000/= kwa mwaka ni 12,000,000/= kwa mavuno ya mara tatu kwa mwaka kwa ekari.

Gharama hii itaenda juu zaidi ama itapungua kutegemea na idadi ya matunda uliyoyapata katika ekari mmoja na bei ya muuzaji. Hivyo unaweza ukapata faida kubwa zaidi ukiongeza uangalizi wa shamba lako na kufuata utaratibu katika ulimaji wa zao hili.

  MAHITAJI

Tikiti maji linahitaji mbolea, maji, kemikali za kuua wadudu na magonjwa pamoja na maandalizi mabali mbali ya shamba ambavyo gharama yake haizidi Tsh. 500,000/= katika uangalizi mkubwa

FAIDA

Hivyo mkulima katika uangalizi wa mzuri ana uhakika wa kupata faida ya Tsh. 3,500,000/=  na zaidi kila baada ya miezi 3-4.  
Ushauri: Kwa mafanikio mazuri na kuinuana kiuchumi wakulima wakiungana na kufanya kilimo bishara watakuwa na nafasi kubwa ya mafanikio kwa maana kiuchumi wanataweza kusaidiana ili kuinua mtaji na kuweza kupata kiasi cha kuanzia shughuli zao za kilimo. 
Share:

Blog Archive

Latest Posts

Translate

Popular Posts

Recent Posts

Unordered List

Pages

Theme Support